Confiar no Senhor
Confiar no Senhor é a base de toda vida espiritual. A confiança em Deus nos livra do medo, nos dá paz e nos posiciona para receber as promessas divinas.
Confiar de todo coração
Confia no Senhor de todo o coração. Não te apoies em teu próprio entendimento — em todos os caminhos o reconheça.
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote
wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
katika njia zako zote mkiri yeye,
naye atayanyoosha mapito yako.
Mungu Mlinzi Wetu
Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,
atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Nitasema kumhusu Bwana, "Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu, ambaye ninamtumaini."
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji,
na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Atakufunika kwa manyoya yake,
chini ya mbawa zake utapata kimbilio,
uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Usalama Wa Watu Wa Mungu
Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.
Hataogopa habari mbaya,
moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema;
Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
Jifurahishe katika Bwana
naye atakupa haja za moyo wako.
Mkabidhi Bwana njia yako,
mtumaini yeye, naye atatenda hili:
Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko,
na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe,
kwa maana wewe Bwana,
hujawaacha kamwe wakutafutao.
Segurança em Deus
Bem-aventurado o homem que confia no Senhor. Ele é como árvore plantada junto às águas — não temerá quando vier o calor.
"Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana,
ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji
uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji.
Hauogopi wakati wa joto ujapo;
majani yake ni mabichi daima.
Hauna hofu katika mwaka wa ukame
na hautaacha kuzaa matunda."
Mtumaini Bwana milele,
kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele.
Hakika Mungu ni wokovu wangu;
nitamtumaini wala sitaogopa.
Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu;
amekuwa wokovu wangu."
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,
heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,
bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu.
Wao wameshushwa chini na kuanguka,
bali sisi tunainuka na kusimama imara.
Ni bora kumkimbilia Bwana
kuliko kumtumainia mwanadamu.
Ni bora kumkimbilia Bwana
kuliko kuwatumainia wakuu.
Não confiar no homem
Não temas — em ti confiarei. Melhor é confiar no Senhor do que confiar no homem ou nos príncipes.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,
katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa.
Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
Lakini mimi ninakutumaini wewe peke yako, Ee Bwana;
nimesema, "Wewe ndiwe Mungu wangu."
Heri mtu yule amfanyaye Bwana kuwa tumaini lake,
asiyewategemea wenye kiburi,
wale wenye kugeukia miungu ya uongo.
Yesu Awatia Moyo Wanafunzi Wake
Yesu akawaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu, mnamwamini Mungu, niaminini na mimi pia.