Pular para o conteúdo
Publicidade

Esperar no Senhor

Por Bíblia Online

Esperar no Senhor é ato de fé e confiança. A Bíblia promete que os que esperam em Deus renovam as forças, recebem direção e experimentam a fidelidade divina no tempo certo.

Renovar as forças

Os que esperam no Senhor renovam as forças. Sobem como águias, correm e não se cansam, caminham e não se fatigam.

bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Ahadi ya Mungu kwa Sayuni

Kwa ajili ya hayo BWANA atangoja, ili awaonee huruma, na kwa ajili ya hayo atatukuzwa, ili awarehemu; kwa maana BWANA ni Mungu wa hukumu; heri wote wamngojao.

Umtumainie BWANA, uwe imara,

Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.

Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA

Katika nchi ya walio hai.

Umtumainie BWANA, uwe imara,

Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.

Wimbo wa ushindi katika Bwana wa Daudi

BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu,

Nimwogope nani?

BWANA ni ngome ya uzima wangu,

Nimhofu nani?

Watenda mabaya waliponikaribia,

Wanile nyama yangu,

Watesi wangu na adui zangu,

Walijikwaa wakaanguka.

Jeshi lijapojipanga kupigana nami,

Moyo wangu hautaogopa.

Vita vijaponitokea,

Hata hapo nitatumainia BWANA.

Neno moja nimelitaka kwa BWANA,

Nalo ndilo nitakalolitafuta,

Nikae nyumbani mwa BWANA

Siku zote za maisha yangu,

Niutazame uzuri wa BWANA,

Na kutafakari hekaluni mwake.

Maana atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya,

Atanisitiri katika sitara ya hema yake,

Na kuniinua juu ya mwamba.

Na sasa kichwa changu kitainuka

Juu ya adui zangu wanaonizunguka.

Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake;

Nitaimba, naam, nitamhimidi BWANA.

Ee BWANA, usikie, kwa sauti yangu ninalia,

Unifadhili, unijibu.

Uliposema, "Nitafuteni uso wangu,"

Moyo wangu umekuambia,

BWANA, uso wako nitautafuta.

Usinifiche uso wako,

Usimkatalie mtumishi wako kwa hasira.

Umekuwa msaada wangu, usinitupe,

Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.

Hata baba yangu na mama yangu wakiniacha,

Bali BWANA atanikaribisha kwake.

Ee BWANA, unifundishe njia yako,

Na kuniongoza katika njia iliyonyoka;

Kwa sababu yao wanaoniotea;

Usinitie katika nia ya watesi wangu;

Maana mashahidi wa uongo wamenijia,

Nao watoao jeuri kama pumzi.

Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA

Katika nchi ya walio hai.

Umtumainie BWANA, uwe imara,

Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.

Espera paciente

Esperei com paciência no Senhor e Ele se inclinou para mim. Confie nele e descanse — Ele agirá no tempo certo.

Shukrani kwa kuponywa na sala ya kutaka msaada

Nilimngoja BWANA kwa subira,

Akaniinamia na kusikia kilio changu.

Akanipandisha toka shimo la uharibifu,

Toka udongo wa utelezi;

Akaisimamisha miguu yangu mwambani,

Akaziimarisha hatua zangu.

Akatia wimbo mpya kinywani mwangu,

Ndio sifa zake Mungu wetu.

Wengi wataona na kuogopa,

Nao watamtumainia BWANA.

Heri aliyemfanya BWANA kuwa tumaini lake,

Wala hakuwaelekea wenye kiburi,

Wala hao wanaogeukia uongo.

Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingi

Miujiza yako na mawazo yako kwetu;

Hakuna awezaye kufananishwa nawe;

Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri,

Ni mengi sana hayahesabiki.

Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,

Umetuzidishia ila masikio,

Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.

Ndipo niliposema, Tazama nimekuja,

(Katika gombo la kitabu nimeandikiwa,)

Kuyafanya mapenzi yako,

Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;

Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.

Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa.

Sikuizuia midomo yangu; Ee BWANA, unajua.

Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;

Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.

Sikuficha fadhili zako wala kweli yako

Katika kusanyiko kubwa.

Nawe, BWANA, usinizuilie rehema zako,

Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima.

Kwa maana mabaya yasiyohesabika

Yamenizunguka mimi.

Maovu yangu yamenipata,

Wala siwezi kuona.

Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu,

Nami nimevunjika moyo.

Ee BWANA, uwe radhi kuniokoa,

Ee BWANA, unisaidie hima.

Waaibike na wafedheheke,

Wote wanaotaka kuniua.

Warudishwe nyuma, watahayarishwe,

Wapendezwao na shari yangu.

Nafsi zetu zinamngoja BWANA;

Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.

Maana mioyo yetu itamfurahia,

Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu.

Ee BWANA, fadhili zako zikae nasi,

Kama tunavyo kutumainia Wewe.

Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja,

Na neno lake nimelitumainia.

Nafsi yangu inamngoja Bwana,

Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi,

Naam, walinzi waingojao asubuhi.

Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa utulivu.

Maana tumaini langu hutoka kwake.

Wewe umngoje BWANA,

Uishike njia yake,

Naye atakutukuza uirithi nchi,

Utawaona Wasio haki wakiangamizwa.

Confiança e perseverança

Confie no Senhor de todo o coração. Sede pacientes na tribulação — o Senhor é fiel e cumprirá todas as suas promessas.

Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,

Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

Katika njia zako zote mkiri yeye,

Naye atayanyosha mapito yako.

Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta subira; na kazi ya subira ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;

mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na subira ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha;

Uvumilivu katika mateso

Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho. Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.

Angalieni, twawaita heri wao waliostahimili. Mmesikia habari za kustahimili kwake Ayubu, kuona mwisho Bwana aliyomtendea, jinsi Bwana alivyo mwingi wa rehema na mwenye huruma.

Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo safi. Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, linalodumu hata milele. Maana,

Mwili wote ni kama majani,

Na fahari yake yote ni kama ua la majani.

Majani hukauka na ua lake huanguka;

Bali Neno la Bwana hudumu hata milele.

Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.

Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyodhani anakawia, bali huwavumilia, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafikie toba.

Mfano wa wanawali kumi

Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi. Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara. Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi. Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki. Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie. Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie. Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi. Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.

Seja o primeiro