Louvor e adoração
O louvor e a adoração são o propósito supremo da vida cristã. A Bíblia está repleta de exortações a louvar o Senhor — com cânticos, instrumentos, danças e com todo o nosso ser.
Louvai ao Senhor!
Todo ser que respira louve ao Senhor! O louvor é o sacrifício agradável que oferecemos continuamente a Deus.
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana.
Msifuni Bwana!
Msifuni Bwana.
Msifuni Mungu katika patakatifu pake,
msifuni katika mbingu zake kuu.
Msifuni kwa matendo yake makuu,
msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,
msifuni kwa kinubi na zeze,
msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
msifuni kwa matoazi yaliayo,
msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana.
Msifuni Bwana!
msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
Na walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Msifuni Bwana.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Na walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake,
anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
Watakatifu washangilie katika heshima hii,
na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Msifuni Bwana.
Msifuni Bwana kutoka mbinguni,
msifuni juu vileleni.
Msifuni, enyi malaika wake wote,
msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi,
msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana,
na ninyi maji juu ya anga.
Vilisifu jina la Bwana
kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.
Aliviweka mahali pake milele na milele,
alitoa amri ambayo haibadiliki milele.
Mtukuzeni Bwana kutoka duniani,
ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,
umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu,
pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,
ninyi milima na vilima vyote,
miti ya matunda na mierezi yote,
wanyama wa mwituni na mifugo yote,
viumbe vidogo na ndege warukao,
wafalme wa dunia na mataifa yote,
ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,
wanaume vijana na wanawali,
wazee na watoto.
Wote na walisifu jina la Bwana,
kwa maana jina lake pekee limetukuka,
utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.
Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Louvor como estilo de vida
Bendirei ao Senhor em todo tempo; o seu louvor estará sempre nos meus lábios. O louvor não depende de circunstâncias.
Nitamtukuza Bwana nyakati zote,
sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Nitamtukuza Bwana nyakati zote,
sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Nitamtukuza Bwana nyakati zote,
sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana,
walioonewa watasikia na wafurahi.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami,
naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote,
nitakusifu zaidi na zaidi.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,
ulinitoa tumboni mwa mama yangu.
Nitakusifu wewe daima.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako,
nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako,
nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha
ninapokuimbia sifa,
mimi, ambaye umenikomboa.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,
jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
Adoração em espírito e verdade
Os verdadeiros adoradores adorarão ao Pai em espírito e em verdade. Deus busca os que o adoram com coração sincero.
Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli."
Njooni, tumwimbie Bwana kwa furaha;
tumfanyie kelele za shangwe
Mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele zake kwa shukrani,
tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.
Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu,
mfalme mkuu juu ya miungu yote.
Mkononi mwake mna vilindi vya dunia,
na vilele vya milima ni mali yake.
Bahari ni yake, kwani ndiye aliifanya,
na mikono yake iliumba nchi kavu.
Njooni, tusujudu, tumwabudu,
tupige magoti mbele za Bwana Muumba wetu,
Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
Mwabuduni Bwana kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Mwabuduni Bwana kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Ingieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya;
mwimbieni Bwana dunia yote.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Bwana aliziumba mbingu.
Fahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake;
dunia yote na itetemeke mbele zake.
A grandeza de Deus
Grande é o Senhor e mui digno de louvor! Sua grandeza é insondável. Os céus declaram sua glória e toda a criação o adora.
Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana,
ukuu wake haupimiki.
Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;
wewe ni sifa ya Israeli.
Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu,
katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni!
Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye!
Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Kwa maana hakupuuza wala kudharau
mateso ya aliyeonewa;
hakumficha uso wake
bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Msifuni Bwana.
Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,
jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema,
liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Bwana anatawala, nchi na ifurahi,
visiwa vyote vishangilie.
Furahini katika Bwana, ninyi mlio wenye haki,
lisifuni jina lake takatifu.
"Mimi ndimi Bwana; hilo ndilo Jina langu!
Sitampa mwingine utukufu wangu
wala sanamu sifa zangu.
Cânticos e instrumentos
Cantai ao Senhor um cântico novo! Louvai com salmos, hinos e cânticos espirituais, fazendo melodia no coração ao Senhor.
Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu, siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki;
kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Msifuni Bwana kwa kinubi,
mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Mwimbieni wimbo mpya;
pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;
waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,
wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.
Wengi wataona na kuogopa
na kuweka tumaini lao kwa Bwana.
Ni vyema kumshukuru Bwana
na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako;
kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako;
kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Louvor nas lutas
Paulo e Silas louvaram na prisão e houve terremoto. O louvor é arma espiritual que transforma circunstâncias e derrota o inimigo.
Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema:
"Mshukuruni Bwana
kwa kuwa upendo wake wadumu milele."
Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu na kusema:
"Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi,
nami nitaondoka uchi,
Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa,
jina la Bwana litukuzwe."
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake;
lisifuni jina lake takatifu.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,
bali upendo wake hudumu siku zote.
Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha,
lakini asubuhi kukawa na furaha.
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza,
ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya.
Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?
Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?
Weka tumaini lako kwa Mungu,
kwa sababu bado nitamsifu,
Mwokozi wangu na Mungu wangu.
Nehemia akasema, "Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Bwana. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu."
Gratidão e louvor
Em tudo dai graças. O louvor nasce da gratidão por quem Deus é e pelo que Ele faz. Cada bênção é motivo de adoração.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Vyote vilivyomo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Vyote vilivyomo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
wala usisahau wema wake wote,
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Vyote vilivyomo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
wala usisahau wema wake wote,
akusamehe dhambi zako zote,
akuponya magonjwa yako yote,
aukomboa uhai wako na kaburi,
akuvika taji ya upendo na huruma,
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
wala usisahau wema wake wote,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma,
na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu,
na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake,
wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Katika siku hiyo mtasema:
"Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake;
julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu,
nitakutukuza na kulisifu jina lako,
kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu
umetenda mambo ya ajabu,
mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
Ninakushukuru na kukuhimidi,
Ee Mungu wa baba zangu:
Umenipa hekima na uwezo,
umenijulisha kile tulichokuomba,
umetujulisha ndoto ya mfalme."
A majestade do Rei
Ao nome de Jesus todo joelho se dobrará. A adoração culminará na eternidade, onde os redimidos louvarão ao Cordeiro para sempre.
Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema:
"Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa,
kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu
na heshima na utukufu na sifa!"
Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba:
"Sifa na heshima na utukufu na uweza
ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi
na kwa Mwana-Kondoo,
milele na milele!"
Akasema kwa sauti kubwa, "Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji."
Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:
"Msifuni Mungu wetu,
ninyi watumishi wake wote,
ninyi nyote mnaomcha,
wadogo kwa wakubwa!"
Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:
"Msifuni Mungu wetu,
ninyi watumishi wake wote,
ninyi nyote mnaomcha,
wadogo kwa wakubwa!"
Kwa kuwa imeandikwa:
" ‘Kama vile niishivyo,’ asema Bwana,
‘kila goti litapigwa mbele zangu,
na kila ulimi utakiri kwa Mungu.’ "
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Vida de louvor
O louvor transforma, fortalece a fé e nos conecta com o céu. Quem louva a Deus em toda circunstância experimenta sua presença real.
Mtumikieni Bwana kwa hofu
na mshangilie kwa kutetemeka.
Nitamshukuru Bwana kwa ajili ya haki yake,
na nitaliimbia sifa jina la Bwana Aliye Juu Sana.
Ee Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,
nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
Ee Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,
nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
Nitafurahi na kushangilia ndani yako.
Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.
Bwana asifiwe,
kwa maana amesikia kilio changu
nikimwomba anihurumie.
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu,
moyo wangu umemtumaini yeye,
nami nimesaidiwa.
Moyo wangu unarukaruka kwa furaha
nami nitamshukuru kwa wimbo.
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi,
naye aiandaa njia yake
ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu."
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,
katika Mungu ninatumaini; sitaogopa.
Mwanadamu apatikanaye na kufa,
atanitenda nini?
Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa.
Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Mungu unipendaye.
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai,
midomo yangu itakuadhimisha.
Nitakusifu siku zote za maisha yangu,
na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
Ewe usikiaye maombi,
kwako wewe watu wote watakuja.
Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.
Nilimlilia kwa kinywa changu,
sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
Sifa apewe Mungu,
ambaye hakulikataa ombi langu
wala kunizuilia upendo wake!
Bali wenye haki na wafurahi,
washangilie mbele za Mungu,
wafurahi na kushangilia.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake,
mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu:
jina lake ni Bwana,
furahini mbele zake.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane,
ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake,
mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu:
jina lake ni Bwana,
furahini mbele zake.
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu,
ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,
wanaotembea katika mwanga
wa uwepo wako, Ee Bwana.
Sio kwetu sisi, Ee Bwana, sio kwetu sisi,
bali utukufu ni kwa jina lako,
kwa sababu ya upendo
na uaminifu wako.
Msifuni Bwana, enyi mataifa yote;
mtukuzeni yeye, enyi watu wote.
Kwa kuwa upendo wake kwetu ni mkuu,
uaminifu wa Bwana unadumu milele.
Msifuni Bwana.
Nitakusifu kwa moyo mnyofu
ninapojifunza sheria zako za haki.
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;
uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa
kwa namna ya ajabu na ya kutisha;
kazi zako ni za ajabu,
ninajua hayo kikamilifu.
Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu,
aifundishaye mikono yangu vita,
na vidole vyangu kupigana.
Msifuni Bwana! kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.
Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Nitamsifu Bwana maisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu sifa
wakati wote niishipo.
Lakini Mungu ashukuriwe, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Kristo. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.
alitangulia kutuchagua tuwe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo kwa furaha yake na mapenzi yake mwenyewe. Kwa hiyo tunamsifu Mungu kwa huruma zake kuu alizotumiminia sisi katika Mwanawe Mpendwa.
Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.
Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. Mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni taifa la Mungu. Mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mmepata rehema.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa,
nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana,
katikati ya mataifa;
nitaliimbia sifa jina lako.
Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
Atasema: "Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao.
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo.
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda.
Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
Pigana vile vita vizuri vya imani. Shika uzima wa milele ambao ndio ulioitiwa ulipokiri ule ukiri mzuri mbele ya mashahidi wengi.
Nawaandikia ninyi akina baba,
kwa sababu mmemjua
yeye aliye tangu mwanzo.
Nawaandikia ninyi vijana,
kwa sababu mna nguvu,
na neno la Mungu linakaa ndani yenu,
nanyi mmemshinda yule mwovu.
Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe, wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.