Namoro e sexo
Namoro e sexo são temas que a Bíblia trata com clareza e sem tabus. Deus criou o sexo como bênção dentro do casamento e nos chama à pureza fora dele.
Pureza sexual
A vontade de Deus é a santificação. Cada um saiba controlar seu próprio corpo em santidade e honra, não na paixão do desejo.
Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima; si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.
Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili.
Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu.
Arrependimento e restauração
Bem-aventurado aquele cujo pecado é perdoado. Deus restaura os que se arrependem e cria neles um coração limpo e renovado.
Shangwe kwa kusamehewa
Heri aliyesamehewa dhambi,
Na kuondolewa makosa yake.
Heri ambaye BWANA hamhesabii hatia,
Na ambaye rohoni mwake hamna hila.
Nilipokosa kuungama dhambi zangu, mifupa yangu ilipooza
Kwa kulia kwangu mchana kutwa.
Kwa maana mchana na usiku
Mkono wako ulinilemea.
Jasho langu likakauka hata nikawa
Kama nchi kavu wakati wa kaskazi.
Ndipo nikakuungamia dhambi yangu,
Wala sikuuficha upotovu wangu.
Nilisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA,
Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.
Kwa hiyo, hebu kila akuaminiye
Akuombe awapo katika dhiki.
Hakika maji makuu yafurikapo,
Hayatamfikia yeye.
Unioshe kabisa uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu.
Maana nimejua mimi makosa yangu
Na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,
Na kufanya maovu mbele za macho yako.
Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo,
Na kuwa safi utoapo hukumu.
Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,
Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
Unifanye kusikia furaha na shangwe,
Mifupa uliyoiponda ifurahi.
Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;
Uzifute hatia zangu zote.
Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Uifanye upya na kuithibiti roho yangu.
Usinitenge na uso wako,
Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
Unirudishie furaha ya wokovu wako;
Unitegemeze kwa roho ya upendo.