Pular para o conteúdo
Publicidade

Palavras de consolo

Por Bíblia Online

A Bíblia é repleta de palavras de consolo para os aflitos. Deus está perto dos que sofrem e promete enxugar toda lágrima, renovar a esperança e restaurar o coração partido.

Deus está conosco

O Senhor é refúgio e fortaleza. Mesmo no vale da sombra da morte, não precisamos temer — Ele está ao nosso lado para nos consolar.

Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti,

Sitaogopa mabaya;

Kwa maana Wewe upo pamoja nami,

Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

Wimbo wa ushindi katika Bwana wa Daudi

BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu,

Nimwogope nani?

BWANA ni ngome ya uzima wangu,

Nimhofu nani?

BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa,

Naam, ngome kwa nyakati za shida.

Neno moja nimelitaka kwa BWANA,

Nalo ndilo nitakalolitafuta,

Nikae nyumbani mwa BWANA

Siku zote za maisha yangu,

Niutazame uzuri wa BWANA,

Na kutafakari hekaluni mwake.

Maana atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya,

Atanisitiri katika sitara ya hema yake,

Na kuniinua juu ya mwamba.

Maana ndiwe tegemeo langu, Ee Bwana MUNGU,

Tumaini langu tokea ujana wangu.

Consolação e esperança

Deus consola os humildes e exalta os abatidos. Ele nunca nos desamparará.

Naye BWANA, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.

Msiwache, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye awapiganiaye.

Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.

Awainuaye juu hao walio chini;

Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.

Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,

Descanso e renovação

Bem-aventurados os que choram, pois serão consolados. A Bíblia nos convida a descansar nos braços do Pai e encontrar paz para a alma.

Heri wenye huzuni;

Maana hao watafarijika.

Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Unifanyie ishara ya wema,

Wanichukiao waione na kuaibishwa.

Kwa kuwa Wewe, BWANA,

Umenisaidia na kunifariji.

Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu,

Kulingana na ahadi yako kwa mtumishi wako.

Ulalapo hutaona hofu;

Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu.

Kila jambo na wakati wake

Kwa kila jambo kuna majira yake,

Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;

Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa kilichopandwa;

Wakati wa kuua, na wakati wa kuponya;

Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;

Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;

Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;

Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;

Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;

Wakati wa vita, na wakati wa amani.

Seja o primeiro