34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.
35 Mlilieni, "Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe.
Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa,
ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,
na kushangilia katika sifa zako."
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele.
Nao watu wote wakasema, "Amen," na "Msifuni Bwana."