Pular para o conteúdo
Publicidade

1 Wafalme 1

11 Ndipo Nathani akamuuliza Bathsheba, mama yake Solomoni, "Je, hujasikia kwamba Adoniya, mwana wa Hagithi, amekuwa mfalme pasipo bwana wetu Daudi kujua jambo hili? 12 Sasa basi, acha nikushauri jinsi utakavyookoa uhai wako mwenyewe na uhai wa mwanao Solomoni. 13 Ingia kwa Mfalme Daudi na umwambie, Bwana wangu mfalme, je hukuniapia mimi mtumishi wako: "Hakika mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme"? Kwa nini basi Adoniya amekuwa mfalme?

Veja também