5 "Mawimbi ya mauti yalinizunguka,
mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka,
mitego ya mauti ilinikabili.
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana,
nilimlilia Mungu wangu.
Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu,
kilio changu kikafika masikioni mwake.