Pular para o conteúdo
Publicidade

Ufunuo 19

Shangwe Huko Mbinguni

1 Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:

"Haleluya!

Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,

2 kwa maana hukumu zake

ni za kweli na za haki.

Amemhukumu yule kahaba mkuu

aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.

Mungu amemlipiza kisasi

kwa ajili ya damu ya watumishi wake."

3 Wakasema tena kwa nguvu:

"Haleluya!

Moshi wake huyo kahaba unapanda juu

milele na milele."

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também