Shangwe Huko Mbinguni
1 Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:
"Haleluya!
Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,
2 kwa maana hukumu zake
ni za kweli na za haki.
Amemhukumu yule kahaba mkuu
aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.
Mungu amemlipiza kisasi
kwa ajili ya damu ya watumishi wake."
3 Wakasema tena kwa nguvu:
"Haleluya!
Moshi wake huyo kahaba unapanda juu
milele na milele."