4 Vizazi huja na vizazi hupita,
lakini dunia inadumu milele.
5 Jua huchomoza na jua huzama,
nalo huharakisha kurudi mawioni.
6 Upepo huvuma kuelekea kusini
na kugeukia kaskazini,
hurudia mzunguko huo huo,
daima ukirudia njia yake.
7 Mito yote hutiririka baharini,
hata hivyo bahari kamwe haijai.
Mahali mito inapotoka,
huko hurudi tena.