Mafundisho Kuhusu Watoto Na Wazazi
1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema. 2 "Waheshimu baba yako na mama yako," hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi, 3 "upate baraka na uishi siku nyingi duniani."
4 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.