2 Huko jangwani hiyo jumuiya yote wakawanungʼunikia Mose na Aroni. 3 Waisraeli wakawaambia, "Laiti tungelikufa kwa mkono wa Bwana huko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa."