Pular para o conteúdo
Publicidade

Mwanzo 12

Wito Wa Abramu

1 Bwana akawa amemwambia Abramu, "Ondoka kutoka nchi yako, uache jamii yako na nyumba ya baba yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.

2 "Mimi nitakufanya taifa kubwa

na nitakubariki,

Nitalikuza jina lako,

nawe utakuwa baraka.

3 Nitawabariki wale wanaokubariki,

na yeyote akulaaniye nitamlaani;

na kupitia kwako mataifa yote duniani

yatabarikiwa."

Veja também