6 Abramu akamwambia, "Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi." Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri. 8 Malaika akamwambia, "Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?"
Akamjibu, "Ninamkimbia bibi yangu Sarai."