5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema,
"Kamwe sitakuacha,
wala sitakupungukia."
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri,
"Bwana ni msaada wangu; sitaogopa.
Mwanadamu anaweza kunitenda nini?"