Pular para o conteúdo
Publicidade

Ayubu 38

4 "Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?

Niambie, kama unafahamu.

5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?

Hakika wewe unajua!

Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?

6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,

au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,

7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,

na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?

8 "Ni nani aliyeifungia bahari milango

ilipopasuka kutoka tumbo,

9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,

na kuyafungia katika giza nene,

10 nilipoamuru mipaka yake,

na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,

11 niliposema, Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi;

hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea?

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também