12 "Lakini hekima inaweza kupatikana wapi?
Ufahamu unakaa wapi?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake;
haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’;
bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote,
wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri,
kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo,
wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa;
thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,
wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 "Ni wapi basi hekima itokako?
Ufahamu hukaa wapi?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai,
imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Uharibifu na Mauti husema,
‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’