46 Naye Maria akasema:
"Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 nayo roho yangu inamfurahia
Mungu Mwokozi wangu,
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili
unyonge wa mtumishi wake.
Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu
amenitendea mambo ya ajabu:
jina lake ni takatifu.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao,
kutoka kizazi hadi kizazi.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake;
amewatawanya wale wenye kiburi
ndani ya mioyo yao.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi,
lakini amewainua wanyenyekevu.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri,
bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli,
kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 Abrahamu na uzao wake milele,
kama alivyowaahidi baba zetu."