Pular para o conteúdo
Publicidade

Lucas 10

Mfano Wa Msamaria Mwema

25 Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, "Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?"

26 Yesu akamjibu, "Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?"

27 Akajibu, " Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; tena, Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ "

28 Yesu akamwambia, "Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi."

29 Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, "Jirani yangu ni nani?"

30 Yesu akamjibu akasema, "Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa. 31 Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani. 32 Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani 33 Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia. 34 Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza. 35 Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbili10:35 Dinari mbili ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku mbili. akampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.

36 "Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?"

37 Yule mtaalamu wa sheria akajibu, "Ni yule aliyemhurumia."

Ndipo Yesu akamwambia, "Nenda, ukafanye vivyo hivyo."

Veja também