Pular para o conteúdo
Publicidade

Lucas 19

2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo. 3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo. 4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.

5 Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!" 6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.

7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, "Amekwenda kuwa mgeni wa mtu mwenye dhambi.’ "

8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, "Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango."

Veja também