Yesu Awaita Wanafunzi Wanne
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi. 17 Yesu akawaambia, "Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu." 18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.