Publicidade

Marcos 10

Yesu Amponya Kipofu Bartimayo

46 Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada. 47 Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"

48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, "Mwana wa Daudi, nihurumie!"

49 Yesu akasimama na kusema, "Mwiteni."

Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, "Jipe moyo! Inuka, anakuita." 50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.

51 Yesu akamuuliza, "Unataka nikufanyie nini?"

Yule kipofu akajibu, "Mwalimu, nataka kuona."

52 Yesu akamwambia, "Nenda zako, imani yako imekuponya." Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-