Yesu Alaani Mtini Usiozaa
12 Kesho yake walipokuwa wakitoka Bethania, Yesu alikuwa na njaa. 13 Akauona mtini kwa mbali, naye akaenda ili aone kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, akakuta una majani tu, kwa kuwa hayakuwa majira ya tini. 14 Akauambia ule mti, "Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako." Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo.