Kuja Kwa Mwana Wa Adamu
24 "Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki,
" ‘jua litatiwa giza
nao mwezi hautatoa nuru yake;
25 nazo nyota zitaanguka kutoka angani,
na nguvu za anga zitatikisika.’
26 "Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu. 27 Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.