Pular para o conteúdo
Publicidade

Marko 3

Mtu Aliyepooza Mkono Aponywa

1 Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono. 2 Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki. 3 Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Njoo hapa mbele ya watu wote."

4 Kisha Yesu akawauliza, "Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?" Lakini wao wakanyamaza kimya.

5 Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, "Nyoosha mkono wako." Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também