22 Binti yake Herodia alipoingia na kucheza, akamfurahisha Herode pamoja na wageni wake walioalikwa chakulani.
Mfalme Herode akamwambia yule binti, "Niombe kitu chochote utakacho, nami nitakupa." 23 Tena akamwahidi kwa kiapo, akamwambia, "Chochote utakachoomba nitakupa, hata kama ni nusu ya ufalme wangu."
24 Yule binti akatoka nje, akaenda kumuuliza mama yake, "Niombe nini?"
Mama yake akamjibu, "Omba kichwa cha Yohana Mbatizaji."
25 Yule binti akarudi haraka kwa mfalme, akamwambia, "Nataka unipe sasa hivi kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia."
26 Mfalme akasikitika sana, lakini kwa sababu alikuwa ameapa viapo mbele ya wageni wake, hakutaka kumkatalia. 27 Mara mfalme akatuma askari mmojawapo wa walinzi wake kukileta kichwa cha Yohana. Akaenda na kumkata Yohana kichwa humo gerezani, 28 akakileta kichwa chake kwenye sinia na kumpa yule msichana, naye yule msichana akampa mama yake.