10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, "Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?"
11 Yesu akawaambia, "Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa? 12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato."
13 Ndipo akamwambia yule mtu, "Nyoosha mkono wako." Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.