Pular para o conteúdo
Publicidade

Mateus 13

14 Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema:

" Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa;

na pia mtatazama lakini hamtaona.

15 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu;

hawasikii kwa masikio yao,

na wamefumba macho yao.

Wasije wakaona kwa macho yao,

na wakasikiliza kwa masikio yao,

wakaelewa kwa mioyo yao,

na kugeuka nami nikawaponya.

16 Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.

Veja também