Pular para o conteúdo
Publicidade

Mathayo 15

3 Yesu akawajibu, "Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? 4 Kwa maana Mungu alisema, Waheshimu baba yako na mama yako,na, Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe. 5 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu, 6 basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu. 7 Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:

8 " Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

9 Huniabudu bure;

nayo mafundisho yao

ni maagizo ya wanadamu tu.’ "

Veja também