Petro Amkiri Yesu Kuwa Ni Mwana Wa Mungu
13 Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, "Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?"
14 Wakamjibu, "Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii."
15 Akawauliza, "Je, ninyi mnasema mimi ni nani?"
16 Simoni Petro akamjibu, "Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai."