Publicidade

Mateus 20

Yesu Awaponya Vipofu Wawili

29 Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu ulimfuata. 30 Vipofu wawili walikuwa wameketi kando ya barabara. Waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele wakisema, "Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie!"

31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, "Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie."

32 Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"

33 Wakamjibu, "Bwana, tunataka kuona."

34 Yesu akawahurumia na kuwagusa macho yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao wakamfuata.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-