Pular para o conteúdo
Publicidade

Provérbios 1

Utangulizi: Kusudi Na Kiini

1 Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:

2 Kwa kupata hekima na nidhamu;

kwa kufahamu maneno ya busara;

3 kwa kujipatia nidhamu na busara,

kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;

4 huwapa busara wajinga,

maarifa na akili kwa vijana;

5 wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,

wenye kupambanua na wapate mwongozo;

6 kwa kufahamu mithali na mifano,

misemo na vitendawili vya wenye hekima.

Veja também