Publicidade

Provérbios 2

Faida Za Hekima

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu

na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

2 kutega sikio lako kwenye hekima

na kuweka moyo wako katika ufahamu,

3 na kama ukiita busara

na kuita kwa sauti ufahamu,

4 na kama utaitafuta kama fedha

na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana

na kupata maarifa ya Mungu.

6 Kwa maana Bwana hutoa hekima,

na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-