23 Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,
maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24 Epusha kinywa chako na ukaidi;
weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
25 Macho yako na yatazame mbele,
kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
26 Sawazisha mapito ya miguu yako
na njia zako zote ziwe zimethibitika.
27 Usigeuke kulia wala kushoto;
epusha mguu wako na ubaya.