3 Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba
hudondoza asali,
na maneno ya kinywa chake
ni laini kuliko mafuta;
4 lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,
mkali kama upanga ukatao kuwili.
5 Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;
hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.
6 Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;
njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.