Pular para o conteúdo
Publicidade

Mithali 5

3 Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba

hudondoza asali,

na maneno ya kinywa chake

ni laini kuliko mafuta;

4 lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,

mkali kama upanga ukatao kuwili.

5 Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;

hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.5:5 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

6 Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;

njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.

7 Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

msiache ninalowaambia.

8 Njia zenu ziwe mbali naye,

msiende karibu na mlango wa nyumba yake,

9 usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine

na miaka yako kwa aliye mkatili,

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também