3 Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba
hudondoza asali,
na maneno ya kinywa chake
ni laini kuliko mafuta;
4 lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,
mkali kama upanga ukatao kuwili.
5 Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;
hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.
6 Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;
njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
7 Sasa basi wanangu, nisikilizeni;
msiache ninalowaambia.
8 Njia zenu ziwe mbali naye,
msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
9 usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine
na miaka yako kwa aliye mkatili,