32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;
yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
33 Mapigo na aibu ni fungu lake
na aibu yake haitafutika kamwe;
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,
naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
35 Hatakubali fidia yoyote;
atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.