Publicidade

Sofonias 1

Siku Kubwa Ya Bwana

14 "Siku kubwa ya Bwana iko karibu:

iko karibu na inakuja haraka.

Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana

kitakuwa kichungu,

hata shujaa atapiga kelele.

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu,

siku ya fadhaa na dhiki,

siku ya uharibifu na ukiwa,

siku ya giza na utusitusi,

siku ya mawingu na giza nene,

16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita

dhidi ya miji yenye ngome

na dhidi ya minara mirefu.

17 Nitawaletea watu dhiki,

nao watatembea kama vipofu,

kwa sababu wametenda dhambi

dhidi ya Bwana.

Damu yao itamwagwa kama vumbi

na matumbo yao kama taka.

18 Fedha yao wala dhahabu yao

hazitaweza kuwaokoa

katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana.

Katika moto wa wivu wake

dunia yote itateketezwa,

kwa maana ataleta mwisho

wa wote wanaoishi katika dunia ghafula."

Veja também

Publicidade
Sofonias
Ver todos os capítulos de Sofonias
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-28_14-13-17-