7 2 Kor 5:1;Mdo 9:15Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu. 8 2 Kor 1:8;7:5Pande zote twateseka, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; 9 twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi; 10 1 Kor 15:31siku zote twabeba katika mwili kuuawa kwake Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu. 11 Rum 8:36Kwa maana sisi tulio hai, siku zote twatolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu ipatikanayo na mauti.
Publicidade