Pular para o conteúdo
Publicidade

2 Coríntios 6

4 2 Kor 4:2bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika subira nyingi, katika mateso, katika shida, katika matatizo; 5 Mdo 16:23;2 Kor 11:23-27katika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika taabu, katika kukesha, katika kufunga; 6 1 Tim 4:12katika kuwa safi, katika elimu, katika uvumilivu, katika utu wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo usio unafiki; 7 1 Kor 2:4katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kulia na za mkono wa kushoto; 8 kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli; 9 2 Kor 4:10;Zab 118:18kama wasiojulikana, bali wajulikanao sana; kama wanaokufa, kumbe tu hai; kama wanaorudiwa, bali wasiouawa; 10 Flp 4:12,13kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote.

Veja também