Uovu katika siku za mwisho
1 1 Tim 4:1Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Rum 1:29Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, 4 Flp 3:19wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; 5 Mt 7:15,21;Rum 2:20;Tit 1:16walio na utaua kwa nje, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.