11 Eze 1:1;Zab 96:13;Isa 11:4;Ufu 3:14Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. 12 Dan 10:6;Ufu 1:14;2:18;3:12Na macho yake yalikuwa kama muali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. 13 Isa 63:1;Yn 1:1Naye amevikwa vazi lililoloweshwa katika damu, na jina lake anaitwa, Neno la Mungu. 14 Ufu 17:14Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. 15 Zab 2:9;Isa 11:4;63:3;Yoe 3:13;Ufu 14:20;12:5Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili kwa upanga huo awapige mataifa. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. 16 Kum 10:17;Dan 2:47;Ufu 17:14;1 Tim 6:15Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.
Publicidade
Apocalipse 19
Wapandaji wa farasi mweupe