30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma kitabu cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma? 31 Yn 16:13Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye. 32 Isa 53:7-8Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili,
Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo,
Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake yule amkataye manyoya,
Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.