Kila jambo na wakati wake
1 Mhu 8:6Kwa kila jambo kuna majira yake,
Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Mwa 47:29;Ayu 7:1;Isa 38:1;Yn 11:14;Ebr 9:27Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;
Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa kilichopandwa;
3 Mwa 9:6;1 Sam 2:6;Hos 6:1,2Wakati wa kuua, na wakati wa kuponya;
Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Kut 15:20;2 Sam 6:16;Zab 149:3Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;
Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;
Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;
Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 Amo 5:13Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;
Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 Lk 14:26Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;
Wakati wa vita, na wakati wa amani.