Pular para o conteúdo
Publicidade

Eclesiastes 3

Kila jambo na wakati wake

1 Mhu 8:6Kwa kila jambo kuna majira yake,

Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2 Mwa 47:29;Ayu 7:1;Isa 38:1;Yn 11:14;Ebr 9:27Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;

Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa kilichopandwa;

3 Mwa 9:6;1 Sam 2:6;Hos 6:1,2Wakati wa kuua, na wakati wa kuponya;

Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

4 Kut 15:20;2 Sam 6:16;Zab 149:3Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;

Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;

Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;

Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

7 Amo 5:13Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;

Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

8 Lk 14:26Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;

Wakati wa vita, na wakati wa amani.

Veja também