28 Ebr 11:20;Kum 33:13,28;2 Sam 1:21;Hes 18:12;Zab 65:9;Zek 9:17Mungu na akupe ya umande wa mbingu,
Na manono ya nchi,
Na wingi wa nafaka na mvinyo.
29 Mwa 9:25;12:3;49:8;Hes 24:9Mataifa na wakutumikie
Na makabila wakusujudie,
Uwe bwana wa ndugu zako,
Na wana wa mama yako na wakusujudie.
Alaaniwe yeyote yule atakayekulaani,
Na abarikiwe yeyote yule atakayekubariki.