Pular para o conteúdo
Publicidade

Lucas 1

Unabii wa Zekaria

67 Na Zakaria, baba yake, akajazwa Roho Mtakatifu, akatabiri, akisema,

68 Lk 7:16;Zab 41:13;72:18Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

Kwa kuwa amewajia watu wake, na kuwakomboa.

69 1 Sam 2:10;Zab 18:2;132:17Ametusimamishia pembe ya wokovu

Katika mlango wa Daudi, mtumishi wake.

70 Kama alivyosema tangu mwanzo

Kwa kinywa cha manabii wake watakatifu;

71 Zab 106:10Tuokolewe na adui zetu

Na mikononi mwao wote wanaotuchukia;

72 Zab 105:8;106:45;Mwa 17:7;Law 26:42Ili kuwatendea rehema baba zetu,

Na kulikumbuka agano lake takatifu;

73 Mwa 22:16,17;Mik 7:20Kiapo alichomwapia Abrahamu, baba yetu,

74 Tit 2:12,14Ya kwamba atatujalia sisi,

Tuokoke mikononi mwa adui zetu,

Na kumwabudu pasipo hofu,

75 Kwa utakatifu na kwa haki

Mbele zake siku zetu zote.

76 Mal 3:1;Mt 3:3Nawe, mtoto, utaitwa nabii wake Aliye Juu,

Kwa maana utatangulia mbele za uso wa Bwana umtengenezee njia zake;

77 Yer 31:34Uwajulishe watu wake wokovu,

Kwa kusamehewa dhambi zao.

78 Hes 24:17;Isa 60:1,2;Mal 4:2Kwa njia ya rehema za Mungu wetu,

Ambazo kwa hizo mwangaza utokao juu umetufikia,

79 Isa 9:2;58:8;Mt 4:16Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti,

Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.

Veja também