Ombi la Yakobo na Yohana
35 Mt 20:20-28Na Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakamwendea, wakamwambia, Mwalimu, twataka utufanyie lolote tutakalokuomba. 36 Akawaambia, Mwataka niwafanyie nini? 37 Wakamwambia, Utujalie sisi tuketi, mmoja mkono wako wa kulia, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika utukufu wako.