3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huivunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? 4 Kut 20:12;21:17;Kum 5:16;Law 20:9Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe. 5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, chochote kikupasacho nikusaidie kwacho nakitoa wakfu, 6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu. 7 Isa 29:13Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,
8 Isa 29:13Watu hawa huniheshimu kwa midomo;
Ila mioyo yao iko mbali nami.
9 Nao waniabudu bure,
Wakifundisha mafundisho
Yaliyo maagizo ya wanadamu.