14 Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: "Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.15 Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?16 Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:17 Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
Publicidade
Atos 2
Veja também
Publicidade