29 "Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.

30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,

31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:

32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."